Falcao atamani kuendelea kukipiga na Manchester United
Na Florence George
Mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia Radamel Falcao ambaye yupo kwa mkopo wa mwaka mmoja katika kikosi cha Manchester United amesema kuwa anataka kuendelea kukipiga katika timu hiyo yenye maskani yake katika dimba la Old Trafford ikitegemeana amecheza muda gani katika timu hiyo na kwa kiasi gani timu hiyo inamuhitaji.
Mchezaji huyo amekuwa akisumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara na kutokuwa katika kiwango cha juu tangu alipotua katika timu hiyo.Tangu mwezi October Falcao ameanza mechi tatu tu za ligi kuu nchini Uingereza huku akifunga goli moja tu hadi sasa.
Kabla ya mechi dhidi ya Liverpool siku ya jumapili Kocha wa Manchester United Louis Van Gaal alisema kuwa Falcao alikuwa fiti kuanza mechi ile lakini mchezaji huyo aliingia akitokea benchi dakika 12 kabla ya mchezo kuisha kuchukua nafasi ya Wayne Rooney.
United wananafasi ya kumsajili moja kwa moja mshambuliaji huyo majira ya joto mwakani ambapo bado wanasubiri kumuangalia mchezaji huyo kama atarudi katika kiwango chake cha awali au la.
Mchezaji huyo amekuwa akisumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara ambapo mwezi January aliumia kifundo cha mguu kilichosababisha akose fainali za kombe la dunia Nchini Brazil.
0 comments:
Post a Comment