Searching...
Image and video hosting by TinyPic
29 August 2013
Thursday, August 29, 2013

NIONAVYO MIMI KWA WAHESHIMIWA WABUNGE

.

Bunge letu la sasa linaidadi kubwa ya wabunge ambao ni vijana,wanapenda MUZIKI na MPIRA.Cha ajabu hakuna hata mmbunge mmoja ambaye anamiliki timu hata ya daraja la 2.Ni kweli vijana wengi hawajasoma,lakini kupitia mpira wanaweza kupata ajira.

Wabunge wengi wamekua na tabia ya kuanzisha ligi za kugombania MBUZI,NG'OMBE,KUKU katika majimbo yao au kikombe ambacho kinathamani ya shilingi elfu 80 na wengine huanzisha mashindano ya kugombania JEZI.Jamani huu sio muda wa kutumia mpira ili kupata NYAMA,mpira ni kazi.

Wabunge kutokana na nafasi yenu,mnaweza kupata wafadhili kibao na mpira mikoani ukarudi.Badala ya kuprint tisheti na mabango mengi wakati wa kampeni,ukiwa na timu JIMBONI kwako ambayo itakuja kutambulika nchi nzima ni KAMPENI tosha,huna haja ya kutengeneza mabango yakujinadi.

issue sio KILIMO KWANZA TU,mkulima aende shamba,msanii afanye sanaa yake na mwana michezo aende kwenye michezo.Huwezi inua michezo kwa zawadi ya MBUZI wala NGO'MBE tu.Tunahitaji wabunge muangalie mbele zaidi.

Tuna hitaji tupate LEKA TUTIGITE nyingi kwenye soka pia.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!