Searching...
Image and video hosting by TinyPic
19 September 2013
Thursday, September 19, 2013

HARUNA NIYONZIMA HANA TATIZO NA MTU.


Jana hakukua na mayai matatu yalioandikwa kiarabu,hakukuwa na kupigwa chupa na mawe,hakukuwa na mashabiki walioleta vurugu,hakukuwa na dege waliopita golini kwa YANGA lakini matokeo ni 1-1!!

Uwanja mbovu wa SOKOINE ambao wazaliwa wa Tanzania unawashinda,mnyarwanda NINYONZIMA alikuwa anautumia kwa madoido kama yuko SANTIAGO BERNABEU!!

Prison hawakuwa na sapoti toka kwa shabiki yoyote,walichofanya ni kumkimbiza mwizi kimya kimya.Ningekuwa na pesa ningemuita NIYONZIMA aje kuuchezea mpira sebuleni kwangu then aseme anataka shilingi ngapi,bonge la fundi huyu jamaa.

TWITE alichokifanya kwenye mechi hizi mbili ambacho nitakumbuka ni kurusha mpira toka MSAMVU hadi UBUNGO BUS TERMINAL.kwa hapa mbeya ni ILOMBA mpaka UYOLE,basi.

i'm sorry!

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!