Searching...
Image and video hosting by TinyPic
21 June 2013
Friday, June 21, 2013

TIOTE APANDISHWA KIZIMBANI ENGLAND KWA KUTUMIA LESENI FEKI YA UDEREVA



NYOTA wa Newcastle United, Cheick Tiote amepandishwa kizimbani kwa mashitaka matano, ikiwemo kutumia leseni feki ya udereva na kudanganya.
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ivory Coast, aliyetimiza miaka 27 jana, anatuhimiwa kutumia leseni feki ya udereva ya Ubelgiji na kufanya jithada za kupata leseni ya Uingereza.
 
Tiote, aliyesajiliwa The Magpies kutoka FC Twente ya Uholanzi mwaka 2010, alisimamishwa na Polisi wa Northumbria karibu na Uwanja wa mazoezi wa klabu yake Februari 12 kwa kushukiwa kudanganya juu ya udereva wake.
Cheick Tiote
Kanjanja: Tiote, akiwasili mahakamani
Cheick Tiote
Mashitaka: Mchezaji wa Newcastle anakabiliwa na mashitaka matano

Gari la kiungo huyo, aina ya Chevrolet Camaro, lenye thamani ya Pauni 75,000, lilifikishwa kituo cha Polisi  alipokamatwa.
Tiote sasa atatakiwa kufika rufaa katika Mahakama Kuu ya Newcastle Julai 5.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!