Searching...
Image and video hosting by TinyPic
27 February 2015
Friday, February 27, 2015

Mizengwe wanayokumbana nayo Azam Fc nchini Sudan.


Azam FC leo saa mbili usiku itajitupa kwenye uwanja wa AlMerrikh kukwaana na Al Merrikh SC.
Azam FC ambayo ilitua hapa Khartoum Jumanne 24/2/2015 imekuwa katika hali nzuri tangia kuwasili. Vijana wa kitanzania wanaosoma hapa Khartoum wamekuwa wenyeji wetu.
Azam FC imekodi Apartment nzima, tumekuwa tukiishi kama nyumbani, tunapika wenyewe, tuna ulinzi wa kutosha wa kambi, na walinzi wetu ambao tumesafiri nao toka Dar es Salaam wakiongozwa na afisa wa usalama wa Taifa wamekuwa wakifanya doria masaa 24.
Tulipowasili Khartoum, wapinzani wetu walijaribu kucheza mchezo mchafu wa kutuchanganya kisaikolojia kwa kuleta mabasi mawili mabovu kutupolea lakini walishangazwa kuona Azam FC ikiachana na basi lao na kupanda basi lingine zuri lililoandaliwa na viongozi wa Azam FC waliotangulia siku tatu kabla.
Jana wakati timu inaenda kufanya mazoezi uwanjani mashabiki wa Merrikh walijipanga barabarani na kurusha vumbi, makopo, mawe nk lakini polisi waliokuwa kwenye magari maalum wakisaidiwa na wanajeshi walifanikiwa kuwadhibiti.
Wenyeji wanasema mashabiki wa Merrikh ni wakorofi na wamekuwa na kawaida ya kufanya fujo kwa timu ngeni.
Benchi la ufundi la Azam FC linaloongozwa na Joseph Omog limesema hawana wasiwasi kabisa kwani wamewaandaa vijana kwa ajli ya mchezo wa leo.

Taarifa hii ni kwa mujibu wa ukurasa wa Facebook wa klabu ya Azam.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!