Searching...
Image and video hosting by TinyPic
26 June 2013
Wednesday, June 26, 2013

ZINEDINE ZIDANE ATEULIWA KOCHA MSAIDIZI WA REAL MADRID - ATAMBULISHWA PAMOJA NA CARLO ANCELOTTI





Real Madrid wamemtambulisha rasmi kocha wao mpya Carlo Ancelotti na pia wametangaza kwamba Zinedine Zidane na Paul Clement watakuwa ndio makocha wasaidizi.

Ancelotti alitambulishwa kwenye mkutano wa waandishi wa habari kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu na raisi wa klabu hiyo Florentino Perez mapema leo mchana.
 
Ancelotti atasaini rasmi mkataba wa miaka mitatu na Madrid July 3 akitokea Paris St Germain.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!