NIONAVYO MIMI:KUFUATIA UJIO WA EMMANUEL OKWI TENA VPL.
Na Oscar Oscar Jr
Mara nyingi sana nimekuwa nikisema Okwi na Niyonzima ni aina ya wachezaji ambao tunawahitaji VPL.Okwi akiwa simba na Niyonzima akiwa yanga,leo hii wote ndani ya Bus moja!
Yanga watakuwa wametumia pesa nyingi sana kumleta huyu jamaa but kama wataamua kurudisha pesa zao,Okwi anauzika washindwe wao tu.Hii ni zawadi tosha ya xmass kwa mashabiki wa yanga!
Kama Ernie Brandts hatofanya mambo ya Andre Villas Boas,Yanga watafanya vizuri.Okwi anauwezo wakuwavuta fans 30,000 kwa kiingilio cha 5,000 kuja kumuona akitambulishwa tu.
Okwi anauwezo wa kuuza jezi laki moja ndani ya mwezi mmoja na kila jezi tsh 10,000 ndani ya mikoa ya Tanzania.scaff,underwares, n.k za bila idadi.
Lakini kuna uwezekano viongozi wa yanga wakamtambulishia tu airport na mchezo ukawa umekwisha.Watakuwa wanautumia msemo wa Julio "napenda zaidi sifa kuliko pesa"
anyway,okwi welcome back to VPL.
0 comments:
Post a Comment