Searching...
Image and video hosting by TinyPic
8 June 2013
Saturday, June 08, 2013

MARRAKECH HAPATOSHI

                                                  HAWA NDO WAMOROCO
Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars inaingia dimbani leo mjini Marakech Morocco kukwaana vikali na timu ya taifa ya nchi hiyo maarufu kama Simba wa Atlas katika kuwania tiketi ya kufuzu kucheza kombe la dunia huko Brazil 2014.

Timu hizo zinakutana huku kukiwa na kumbukumbu ya ushindi mzito wa Taifa Stars wa 3 - 1 dhidi ya Morocco jijini Dar-es-salaam mwezi March mwaka huu.

Kocha wa Morocco, Rachid Taoussi atawatumia mastaa wake Youssef el Arabi, Adil Hermach, Youness Belhanda na Abderrazak Hamdallah kuitikisa ngome ya Tanzania ambayo nayo itawategemea sana wakali wake wakiongozwa na kipa Juma Kaseja, Mrisho Ngassa, Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta.

Taifa Stars iko nyuma ya Ivory Coast kwenye kundi D, huku Morocco ikifuata kwenye nafasi ya tatu.

Unahisi nini kitatokea pale Stade de Marakech?
                                              
                  TAIFA STARS

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!