Searching...
Image and video hosting by TinyPic
19 March 2014
Wednesday, March 19, 2014

KIONGO WA REAL MADRID NJE MSIMU MZIMA.

Kiungo wa Real Madrid Jese hatoshiriki mechi yeyote msimu huu baada ya kujeruhiwa vibaya katika mechi hiyo dhidi ya Shalke 04.
Jesse mwenye umri wa miaka 21 alianguka vibaya baada ya makabiliano na beki wa Schalke Sead Kolasinac na akalazimika kubebwa kwenye machela daktari akisema ni jereha la goti. 


Kocha wa klabu hicho tajiri duniani Carlo Ancelotti amedhibitisha kuwa Jesse ameumia kiasi cha kuwa amefunga msimu na kuwa klabu hiyo itamsaidia katika matibabu ya jeraha hilo la goti hadi atakaporejea msimu ujao. 

Jesse ameichezea Madrid katika mechi 31 na kuifungia mabao nane, la kwanza likiwa bao dhidi ya mahasimu wao wa jadi Barcelona mwaka uliopita.
Kutokana na ushindi huo mkubwa Madrid sasa inajiunga na Barcelona na Athletico Madrid katika droo ya hatua ijayo ya robo fainali inayotarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa. 

Real vilevile inatarajia kuendeleza msururu wa matokeo mema katika ligi yao ya nyumbani La liga ambapo imeratibiwa kukwaruzana na watani wao wa jadi Barcelona siku ya Jumapili katika mechi inayotizamiwa na mashabiki wengi zaidi duniani ya El -Classico.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!