Borussia Dortmund ilifuzu kwa hatua ya robo fainali
licha ya kuambulia kichapo cha 1-2 mikononi mwa Zenit St Petersburg huko
Ujerumani .
itakuwa kwenye droo ya robo fainali siku ya ijumaa baada ya kusajili ushindi wa jumla ya mabao 5-4.
Zenit, ilikuja Ujerumani ikiwa tayari imemfuta kazi Luciano Spalletti sasa itakuwa chini ya Kocha Andre Villas-Boas kuanzia .
Mchezaji kutoka Brazil ,Hulk ndiye aliyewaweka wageni hao mbele kunako dakika ya 16 lakini Sebastian Kehl akaisawazishia Dortmund kunako dakika ya 38.
Licha ya bao la Jose Rondon 73 st Petersburg haikuweza kusonga mbele.
Dortmund hata hivyo itakuwa na kibarua kigumu katika mkondo wake wa kwanza kwani Marco Reus na nyota wao Robert Lewandowski kuadhibiwa kwa kucheza visivyo .
Lewandowski hatoruhusiwa kushiriki mkondo wa kwanza wa robo fainali.
Dortmund sasa inajiunga na Bayern Munich, Paris Saint Germain, Real Madrid ,Athletico Madrid, Barcelona, Manchester United na Chelsea katika hatua ijayo ya robo fainali.
Droo ya robo fainali itafanyika Ijumaa .
0 comments:
Post a Comment