Searching...
Image and video hosting by TinyPic
15 November 2013
Friday, November 15, 2013

FACEBOOK NA TWITTER ZINAWEZA KUONGEZA RADHA KWENYE SOKA.

NIONAVYO MIMI MTOTO WA TABORA:
FACEBOOK NA TWITTER ZINAWEZA KUONGEZA UTAMU WA SOKA.

Na Oscar Oscar Jr
Klabu za VPL ambazo zinatumia mitandao ya kijamii kama Facebook na Twitter wanakosa ubunifu,ndiyo maana hawana followers wengi online wakati huku mtaani kwenye "Hard copy" wana maelfu ya Fans!!

Unajui kwa nini? Shabiki haoni taarifa mpya na zakuvutia thats why haoni sababu ya ku-like au ku-follow account hizo.hivi leo ukisikia kwamba Haruna Moshi na Jerry Santo watakuwa wanajibu maswali ya mashabiki wao kuanzia saa 2-4 usiku kwenye Twitter account ya Coastal union,utalala? Utaacha ku-like page yao?

Mashabiki wanahamu ya kuwajua wachezaji wao kiundani,wanatamani kujua maisha binafsi ya wachezaji n.k Hivi leo Yanga wakimuweka Manji "live" kwenye Facebook account ya Yanga na kujibu hoja za mashabiki kwa masaa mawili tu,unadhani kunamtu atalala? Unadhani kuna mtu ataacha ku-like ukurasa wao?

Tuwekeni LIVE na wachezaji wetu,tujue mengi kupitia majibu yao.Kazi yenu kubwa kwenye account hizo ni kutuwekea kikosi kitakachoanza na vipicha uchwara!! Hivi Simba mnashindwa nini angalau kumleta Abel Dhaira LIVE tuzungumze naye??

Waleteni wachezaji karibu na mashabiki ili kupunguza hata uongo ambao tunauona kwenye baadhi ya Media.

I'm sorry!

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!