TIMU ya taifa ya Brazil imeshinda mechi
yake ya pili ya Kombe la Mabara, huku kijana mdogo mwenye kipaji cha
ajabu, Neymar akifunga bao tamu ndani ya dakika 10 za kwanza kabla ya
kumtengenezea nafasi ya kufunga bao la pili
Brazil imeilaza Mexico mabao 2-0 bila ubishi na sasa inatimiza ponti sita na kuzidi kujiimarisha kileleni mwa Kundi A.
Daniel Alves alipinda krosi kutoka kulia
na nyota mpya wa Barcelona, Neymar akaitokea wa kwanza mbele ya beki wa
Mexico, kabla ya kuhadaa na kumtungua kipa Jose Corona dakika ya tisa
na dakika ya 90 akampa pande Jo kufunga la pili.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa
Howard Webb wa Uingereza, kikosi cha Brazil kilikuwa: Cesar, Alves,
Silva, Luiz, Marcelo, Luiz Gustavo, Paulinho, Oscar/Hernanes dk62,
Hulk/Lucas Moura dk78, Neymar na Fred.
Mexico:
Corona, Rodriguez, Salcido, Torrado, Dos Santos, Henandez, Moreno,
Guardado, Torres/Barrera dk70, Mier na Flores/Herrera dk68.

Balaa: Neymar alikuwa shujaa wa Brazil leo

Pongezi: Neymar akishangilia bao lake

Javier Hernandez akiwa chini baada ya kukutana na shuluba la Thiago Silva

Damu! David Luiz aliumizwa kichwani na beki mwenzake wa kati, Thiago Silva hadi kutokwa damu

Luiz akitibiwa

Damu ilisababisha abadilishe jezi

Mbio: Neymar akijaribu kumtoka Gerardo Torrado wa Mexico

Hulkl akipambana na Jorge Torres Nilo wa Mexico

Shabiki wa Brazil

Neymar akiugulia maumivu katika moja ya matukio ya mechi hiyo baada ya kuumia
0 comments:
Post a Comment