Searching...
Image and video hosting by TinyPic
21 June 2013
Friday, June 21, 2013

MAN UNITED NA THIAGO ALCANTARA SWAAFI...WAMALIZANA NAYE MBELE YA BABA YAKE



KLABU ya Manchester United iko karibu kabisa kumsajili kiungo wa Barcelona, Thiago Alcantara kwa dau la Pauni Milioni 17.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England wamewapiku wapinzani wao, Manchester City kwa kukubaliana juu ya maslahi binafsi na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22, ambaye watakuwa wanamlipa Pauni Milioni 5 kwa mwaka. Makubaliano yamemhusisha Thiago na baba yake, Mazinho.
 
Sasa wanatakiwa kumalizana na Barcelona na vyanzo vinasema habari rasmi inaweza ikatolewa leo, lakini majadiliano baina ya klabu hizo mbili yataendelea mwishoni mwa wiki.
Incoming: Thiago Alcantara would significantly strengthen Manchester United's midfield
Anakuja: Thiago Alcantara yuko njiani kuelekea Manchester United
Thiago presents Spanish Prime Minister Mariano Rajoy (R) with a signed shirt after Span's Under 21 European Championship triumph
Thiago akimkabidhi Waziri Mkuu wa Hispania, Mariano Rajoy (kulia) jezi aliyoisaini ya timu ya vijana ya Hispania chini ya umri wa miaka 21 baada ya kutwaa ubingwa wa Ulaya

Thiago anatazamwa kama mmoja wa nyota wanaochipukia katika soka ya Hispania na alionyesha makali yake alipofunga Hat-trick wakati U-21 inatwaa ubingwa wa Ulaya wiki hii.
Lakini amekuwa hana furaha kwa kukosa nafasi Nou Camp, licha ya Barca kumuhakikishia atakuwa kinara katika timu yao baadaye.
Talented: Barcelona hoped the midfielder would become a key player for them in the future
Kipaji: Barcelona wanatumai kiungo huyu atakuwa tegemeo lao baadaye
Retired: United need a long-term replacement for Paul Scholes
Mstaafu: United inahitaji mrithi wa muda mrefu wa Paul schoels

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!