Searching...
Image and video hosting by TinyPic
25 June 2013
Tuesday, June 25, 2013

ANDRE SCHURRLE - MCHEZAJI WA KWANZA KUSAJILIWA NA MOURINHO CHELSEA MSIMU HUU - ANGALIA UWEZO WAKE



Jose Mourinho amefungua rasmi akaunti ya Chelsea na kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kijerumani ANDRE SCHURRLE - ambaye leo hii amefaulu vipimo vya afya na kujiunga rasmi na Chelsea akitokea Bayern Leverkusen.

Chelsea wamempa mjerumani huyo mkataba wa miaka mitano, na kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Jose Mourinho tangu arejee kutoka Santiago Bernabeu mapema mwezi uliopita.

Schurrle, 22, alisema: “Nina furaha kusajili hapa. Ni heshima kubwa kwangu kuichezea klabu hii, ninaangalia mbele kuitumikia timu hii.”

Schurrle ana uwezo wa kucheza aidha kama winga au mshambuliaji wa kati akiungana na wachezaji wengine kama  Juan Mata, Eden Hazard, Oscar na Kevin De Bruyne katika kugombea nafasi ya kuwemo katika kikosi cha kwanza cha Mourinho. 

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!