Searching...
Image and video hosting by TinyPic
24 May 2013
Friday, May 24, 2013

hii ni vita nyingine EPL


Carddiff city ni timu ambayo inamilikiwa na mmalasiya VINCENT TAN ambaye amefanikiwa kuipandisha EPL msimu ujao.inatoka kusini mwa Wales ambako pia Swansea city wanatoka.

Swansea city vs Carddiff city ni derby ambayo inasemekana ndo inavurugu kuliko zote kwenye Great Britain.man c vs united haitii maguu wala,arsenal vs Spurs,sunderland vs Newcastle wote wanasubiri kwa hawa jamaa.

Craig Bellamy baada ya kutangatanga EPL aliamua kurudi kwao wales na kuisaidia Carddiff kupanda daraja.big up kwake.Carddiff city ni kama stoke city ya mwaka juzi,wakati swansea wakicheza samba,wao ni buti mwanzo mwisho.

Carddiff city ndo timu pekee kutoka wales ambayo imewahi kutwaa FA cup baada ya kumtandika arsenal,huku wapinzania wao swansea walimkandamiza mtu goli 5 na kutwaa Carling Cup msimu huu.

Kwa sasa wamehama uwanja wao wa nyumbani NINIAN PARK na watatumia CARDDIFF CITY STADIUM.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!