Searching...
Image and video hosting by TinyPic
22 June 2013
Saturday, June 22, 2013

USAJILI BONGO

                                                                     


SI Simba, Yanga na Azam tu, usajili umechanganya kwa klabu zote za Bara kujiandaa na Ligi Kuu itakayoanza Agosti.
Uongozi wa Coastal Union umetuma ofa Simba kumtaka kwa mkopo winga wake wa zamani Uhuru Seleiman na Mkurugenzi wa Ufundi, Nassoro Bin Slim amethibitisha hilo.
Alisema wapo katika hatua za mwisho kukamilisha usajili wa straika wa Bandari ya Kenya, Crispian Odulla na mpaka sasa wachezaji wao wapya ni Haruna Moshi, Juma Nyosso (Simba), Keneth Masumbuko (Polisi Moro), Marcus Ndaheli, Said Rubawa (Oljoro JKT) na Abdullah Othman (Jamhuri ya Pemba)
Mgambo JKT ya Tanga, kocha wao Mohammed Kampira ameweka wazi kuwa wamemsajili straika mkongwe Salim Aziz ‘Gilla’ aliyewika na Simba pamoja na Coastal Union.
Oljoro JKT ya Arusha, Katibu wao Alex Mwamgaya amesema bado wanatafakari kabla ya kuanza usajili wao rasmi kwa ajili ya msimu ujao wa ligi.
Straika matata wa zamani wa Tanzania ambaye sasa ni kocha msaidizi wa Prisons, Oswald Morris anasema bado wapo likizo lakini wamependekeza kusajili wachezaji wapya tisa kwenye ripoti yao.
Mtibwa Sugar wamethibitisha wako kwenye  mazungumzo na Yanga kumtaka beki wa kushoto Stephano Mwasika anayesugua benchi.
Mecky Maxime ambaye ni Kocha wa Mtibwa amesema usajili wao utazingatia zaidi sehemu zilizobomolewa.
                             

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!