Searching...
Image and video hosting by TinyPic
13 April 2015
Monday, April 13, 2015

Barcelona yapata pongezi kutembea Tanzania


Na George Mganga
Balozi wa Uhispania nchini Tanzania, Luis Cuesta amewapongeza wachezaji wa zamani wa klabu ya Barcelona ya Uhispania kwa kufanya ziara nchini Tanzania, huku akisema kuwa udhamini wa Castle Lager kwa FC Barcelona umefungua milango ya ushirikiano kati ya nchi hiyo na klabu hiyo kongwe duniani.
Akizungumza katika hafla ya jioni kwa ajili ya wachezaji wa zamani wa FC Barcelona iliyoandaliwa na Ubalozi wa Uhispania nyumbani kwa balozi jijini Dar es Salaam, Cuesta amesema kwamba ushirikiano wa Castle Lager na FC Barcelona umefungua milango ya fursa mbalimbali kwa Tanzania na klabu hiyo kongwe ikiwemo ziara ya wachezaji wa zamani wa klabu hiyo ambao walikuja nchini kucheza mechi ya kirafiki na wachezaji wa zamani wa Tanzania.
Katika mechi hiyo iliyochezwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam, wachezaji hao wa zamani wa Barcelona walishinda 2-1 dhidi ya wachezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania.
Kwa upande wake, Baloziwa Uholanzi nchini Tanzania, Jaap Frederiks ambaye naye alihudhuria hafla hiyo kwa sababu ya wachezaji wa Kiholanzi wanaochezea Barcelona alisema kwamba amefurahi juu ya ziara hiyo na anawapongeza Castle Lager kwa kuileta Barcelona karibu na Afrika.
“Barcelona ni timu yenye wapenzi duniani kote. Watanzania na nchi nyingine barani Afrika watapata fursa ya kuwaona wachezaji wa timu hii kubwa ikiwa ni jambo zuri na la kihistoria,”alisema.
Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Barcelona, Johan Cruyff pamoja na gwiji wa Barcelona wa zamani Luis Garcia ni kati ya walioudhuria hafla hiyo.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!