Searching...
Image and video hosting by TinyPic
23 October 2014
Thursday, October 23, 2014

Super Mario Balotelli kuadhibiwa.


Na Rossa Kabwine

Rogers baada ya Balotelli kubadilishana jezi Meneja wa Liverpool Brendan Rogers amesema atachukua hatua dhidi ya Baloteli baada ya Balotelli kubadilishana jezi na Pepe mchezajiwa Real Madrid muda wa mapumziko Jumatano katika mchezo wa klabu bungwa Ulaya ambapo liverpool ilifungwa 3-0 na mabingwa watetezi wa kombe hilo uwanja wa Anfield. 


Rogers alisema “ kama unataka kufanya hivyo fanya mwisho wa mchezo. Nikitu ambacho nitakifanyia kazi alhamisi(leo)" Mario Balotelli dakika 45 za kwanza dhidi ya real Madrid alipiga mashuti mawili lakini yote yalizuiwa na walinzi wa Madrid huku akionekana kupiga pasi chache zaidi ya wachezaji wote (17) sawa na Lazar Markovic ambaye alicheza kwa dakika 23 tu.

Rogaers ambaye aligharifika baada ya msimu uliopita kushuhudia mlinzi wake Mamadou Sakho akibadilishana jezi na Samuel Etoo kwenye mchezo wao dhidi ya Chelsea  alisema: “ tulikuwa na hali hii mwaka jana na tuli ishughulikia ndani ya club” 

Rogers pia amemkosoa Mtaliano huyo baada ya Liverpool kucheza chini ya kiwango dhidi ya mabingwa hao wa Ulaya ambao walijipatia goli la kwanza kupitia kwa Cristiano Ronaldo ambaye alifunga goli la 70 katika michuano hiyo na mengine yakifungwa na Karim Benzema. 

Balotelli alitolewa na nafasi yake ilichukuliwa na Adam Lallana baada ya mapumziko.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!