Searching...
Image and video hosting by TinyPic
21 December 2013
Saturday, December 21, 2013

NIONAVYO MIMI:LIVERPOOL WASIMUANGUSHE LUIZ SUAREZ.

Na Oscar Oscar Jr

Katika watu wenye furaha siku ya leo,ni fans wa Liverpool.Baba Delphina,mr Hat-trick,komando Suarez amekubali kusaini mkataba wa kuitumikia Liverpool kwa miaka 5 ijayo!

Suarez ni mchezaji anayestahili UCL ili iwe rahisi pengine kuelekea kwenye Ballon D'or.Liverpool wanatakiwa kumuongezea nguvu.safu ya ushambuliaji,sina tatizo nayo.

Liverpool inamuhitaji mtu mmoja wa aina ya Alex Song au Luiz Gustavo ili kutuliza dimba,inahitaji mtu mwingine wa aina ya Coutinho ili acheze sehemu ya Gerrard ambayo naona jua lake liko machweo!

Lucas sio mzuri sana,Handerson simkubali kabisa kama SAF na Allen,alitakiwa awe kwanza stoke city.Wakipata aina ya Mata au Modric kucheza nafasi ya Gerrard,gari la manzese litakuwa limewaka.

Kwanamna wanavyomvumilia Brendan Rodgers,atawajengea timu bora hivi punde.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!