Tamko La CECAFA Kuhusu Timu Kujitoa Kwenye Michuano.
Baraza la soka kwa nchi za Afrika
Mashariki na kati CECAFA, limesema linaendelea na matayarisho ya
michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na kati maarufu kama kombe la
Kagame itakayoanza kutimua vumbi June 18 huko Darfur nchini Sudan.
Katibu Mkuu wa CECAFA Nicolaus Musonye akizungumza kutokea Nairobi amesema hawana taarifa yeyote ya timu kujitoa katika michuano hiyo na kwamba wao wanaendelea na maandalizi ya mwisho mwisho kabla ya kuanza kwa michuano hiyo.
0 comments:
Post a Comment