Searching...
Image and video hosting by TinyPic
22 June 2013
Saturday, June 22, 2013

PAWASA ALONGA KUHUSU KASSEJA


                                                


BEKI wa zamani wa Simba, Boniface Pawasa amesema klabu hiyo imefanya usajili mzuri mpaka sasa, licha ya kubezwa na baadhi ya wadau lakini amemkingia kifua kipa wa heshima Msimbazi, Juma Kaseja.
“Wengi wanaona kama Simba imefanya usajili wa kiwango cha chini  eti kwa sababu ina wachezaji wengi vijana na wana wasiwasi kuwa timu inaweza kufanya vibaya msimu ujao ila mimi nawaunga mkono kwa usajili waliofanya  na utawabeba,”alisema Pawasa na kushauri Simba itafute beki wa kati.
“Ukiangalia kitu kikubwa kilichoigharimu Simba msimu uliopita hasa hasa ni safu ya ulinzi na hiyo ndiyo inatakiwa kwenye usajili huu ipewe kipaumbele, kwani muda mwingine unaweza ukamlaumu tu kipa Juma Kaseja kumbe safu ya ulinzi imemgharimu. Lazima uangalie muda mwingine kipa anakuwa bora kutokana na uwezo wake au anabebwa na mabeki wake bora, sasa safu ya ulinzi ya Simba haikuwa bora msimu uliopita hivyo hata kipa hataonekana bora.
“Naamini Kaseja ni kipa mzuri na ana uwezo, hayo yote yanayotokea ni upepo tu, haitajiki kuvunjwa moyo kama watu wanavyofanya sasa, yule ni kipa wa timu ya Taifa lazima apewe heshima yake na isitoshe kaichezea Simba muda mrefu na naamini bado ana uwezo wa kucheza kwa kiwango kwa muda mrefu,” 

alisema Pawasa ambaye ni miongoni mwa wachezaji wa zamani wenye taaluma. Simba inadai imemwambia Kaseja aamue anataka kusajiliwa kwa mkataba wa aina gani.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!