Searching...
Image and video hosting by TinyPic
8 April 2015
Wednesday, April 08, 2015

Tanzania yapangwa na wababe kufuzu AFCON 2017


Na George Mganga
Ratiba ya mechi za kwenda kushiriki michuano ya AFCON mwaka 2017 imepangwa leo huku Tanzania ikiwa imepangwa katika kundi G pamoja na wababe ikiwemo mafarao wa Misri halikadhalika Nigeria na Chad katika fainali ambazo zitafanyika huko Gabon.
Droo hiyo imefanyika leo mjini Cairo, Misri huku Gabon ikifanikiwa kuzipiku Ghana na Nigeria kuwa mwenyeji mshirika wa michuano hiyo ya AFCON itakayokuwa ya 31.
Mwaka 2012 Gabon walikuwa washirika wenyeji wa michuano hiyo halikadhalika wenyeji wao Equatorial Guinea.
Makundi ya kufuzu AFCON 2017 yapo hivi;
Kundi A; Tunisia, Togo, Liberia na Djibouti.
Kundi B; DRC, Angola, Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) na Madagascar.
Kundi C; Mali, Equatorial Guinea, Benin na Sudan Kusini.
Kundi D lina timu za Burkina Faso, Uganda, Botswana na Comoros.
Kundi E; Zambia Kongo, Kenya na Guinea Bissau.
Kundi F, Cape Verde, Morocco, Libya na Sao Tome.
Kundi G; Nigeria, Misri, Tanzania na Chad.
Kundi H; Ghana, Msumbiji, Rwanda na Mauritius.
Kundi I; Ivory Coast, Sudan, Sierra Leone na Gabon.
Kundi J; Algeria, Ethiopia, Lesotho na Shelisheli.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!