Searching...
Image and video hosting by TinyPic
28 March 2014
Friday, March 28, 2014

KUFUKUZWA KWA BOBAN NA JUMA NYOSO COASTAL UNION

Na Hafidhi Kido.

Zimezuka taarifa kuwa klabu ya Coastal Union, inayoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, imewatimua wachezaji wake wawili Haruna Moshi ‘Boban’ na Juma Said ‘Nyoso’.
Kwa mujibu wa Katibu wa Coastal Union, Kassim Siagi taarifa hizo hazina ukweli wowote kwani bado klabu ina mkataba na wachezaji hao.


Kumezuka maneno yasiyo na ithibati katika mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari hasa baadhi ya magazeti kuwa wachezaji hao wametimuliwa kikosini kutokana na vitendo vya hujuma wakiwahusisha na kucheza chini ya kiwango katika mechi dhidi ya Azam FC, iliyoisha kwa Wagosi kulala 4-0.


Baada ya hapo ikadaiwa wachezaji hao wametemwa, lakini ukweli ni kuwa kocha wa Coastal Union, ameamua kuwatumia viajana wa kikosi cha pili na baadhi ya wachezaji ambao walikuwa nje kwa muda mrefu.


Maamuzi hayo ya kocha Yusuf Chipo, ni kwa lengo la kuhakikisha Coastal Union inakuwa na sura mpya huku akiendelea kuwatumia wachezaji wakongwe walio katika klabu hiyo kwasababu ya uzoefu.
Kwa mara ya kwanza kutumiwa kwa mfumo huo mpya ilikuwa ni katika mechi dhidi ya Simba katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam, ambapo wagosi waliibuka na ushindi finyu wa bao 1-0 lililoingizwa kimiani na beki wa kulia Hamadi Juma.


Hivyo ieleweke kuwa wachezaji waliotajwa kutimuliwa bado ni wachezaji halali wa Coastal Union na wataendelea kutumika katika mechi nne zilizobaki kwa utaratibu aliouweka kocha.
Angalizo: 


Si vema kuzungumza habari ambazo hazina uhakika, namba ya simu ya msemaji ni 0713 593894. Muda wowote ukiwa na kitu kinakukwaza usichoke kuuliza kwa ufafanuzi Zaidi.
HAFIDH KIDO
MSEMAJI- CUSC.


0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!