Searching...
Image and video hosting by TinyPic
22 March 2014
Saturday, March 22, 2014

WENGER HAENDI KOKOTE

Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amesisitiza nia yake ni kubakia kama kiongozi wa klabu hiyo ya Uingereza kwa muda licha ya kutosaini mkataba mpya na timu hiyo ya London.
Wenger aliongoza mechi yake ya 1000 Jumamosi dhidi ya Chelsea ingawa hatua hiyo iliishia kwa majonzi pale walipoadhibiwa 6-0. 



Meneja huyo amepanga kumaliza sintofahamu ya hatima yake Arsenal kwa kuhakikishia ataendelea kushikilia usukani msimu ujao.
“Ndio, nafikiria hivyo,” alijibu alipoulizwa na wanahabari kama angekuwa mwalimu wa Arsenal msimu ujao. 

“Nataka kupata ufanisi na matarajio ni mengi hapa ingawa kuna wasiwasi inayotanda. Ahadi yangu ni kamili na sina nia ya kuangalia kwingine. Nataka kubakia hapa na hakuna sababu ya kuwa na wasiwasi.
“Hamu yangu ni kubaki hapa.” 

Wenger aliteuliwa kama mwalimu wa klabu hiyo mwaka wa 1996 na ameshinda mataji 11 na timu hiyo lakini hakafanikiwa kutia lolote kibindoni tangu 2005 pale alipoongoza Arsenal kuinua kombe la FA.

0 comments:

Post a Comment

 
Back to top!